Skip to main content

DRC inaishutumu Rwanda kuwasaidia waasi wa M23 katika mashambulizi ya Bunagana

Mamlaka katika eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) ilisema wanajeshi wa Rwanda wakiwa na silaha walisaidia mashambulizi yanayofanywa na kundi la waasi wa M23 siku ya Jumapili huku DRC ikiwashutumu Rwanda kwa kutaka kuuteka mji wa mpakani wa Bunagana.

Ghasia hizo ziliwasukuma zaidi ya watu 25,000 kukimbia eneo hilo huku maelfu wakitorokea nchi jirani ya Uganda shirika la Umoja wa Mataifa la misaada ya kibinadamu (OCHA) lilisema.

Shutuma zinazotolewa na Congo ni sehemu ya mzozo unaoongezeka kati ya majirani hao ambao wamefufua chuki za zamani. Rwanda inakanusha kuunga mkono mashambulizi yanayofanywa na M23.

Ofisi ya gavana wa jimbo la Kivu kaskazini ilisema kuwa vikosi vya Congo vimezuia mashambulizi ya mapema asubuhi Jumapili yaliyofanywa na M23 yakisaidiwa na vikosi vya Rwanda karibu na mji wa Bunagana na kwingineko.

The post DRC inaishutumu Rwanda kuwasaidia waasi wa M23 katika mashambulizi ya Bunagana appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/23779/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT