Skip to main content

CHAMA KARUDI ILA BADO HAJAWA FITI


LICHA ya kuanza mazoezi ndani ya kikosi cha Simba kiungo Clatous Chama bado hajawa fiti kutokana na kukaa nje kwa muda mrefu akitibu majeraha ya enka.

Nyota huyo wa Simba kwa sasa yupo Bongo baada ya kurejea kutoka Zambia Julai 10 ambapo alikuwa huko akipewa matibabu ya enka ambayo aliiumia kwenye mchezo wa dabi dhidi ya Yanga.

Jana,Juni 11 Chama alianza mazoezi kwenye Uwanja wa Mo Arena akiwa chini ya Kaimu Kocha Mkuu, Seleman Matola ikiwa ni kwa ajili ya maandalizi ya mechi zao zijazo za ligi.

Matola amesema kuwa kutokana na kutokuwa kwenye mazoezi kwa muda mrefu kunamfanya asiweze kuwa fiti moja kwa moja hivyo anahitaji muda kuweza kurejea kwenye ubora wake.

Matola amechukua mikoba ya Pablo Franco ambaye alichimbishwa ndani ya kikosi hicho Mei kutokana na kushindwa kufikia malengo ya timu ikiwa ni pamoja na kutwaa Kombe la Shirikisho baada ya kuondolewa na Yanga hatua ya nusu fainali, Mei 28 ambapo Simba ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0.

Mtupiaji wa bao la ushindi alikuwa ni Feisal Salum aliyefunga bao hilo akiwa nje ya 18.

Mbali na kuwa Zambia kwa ajili ya matibabu pia Chama alikuwa kwenye kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha mkewe Mercy Chama aliyetangulia mbele za haki Mei mwaka jana.

The post CHAMA KARUDI ILA BADO HAJAWA FITI appeared first on Saleh Jembe.

The post CHAMA KARUDI ILA BADO HAJAWA FITI appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/FGNVHB6

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT