Skip to main content

Biden alitaka Bunge kusitisha kwa muda kodi ya mafuta ya petroli

Familia za Wamarekani ambazo zinalipa pesa nyingi za mafuta ya petroli zinahitaji afueni ya kifedha, Biden amesema huku akilishinikiza bunge kuchukua hatua, alipoeleza kuwa pendekezo lake la kusitisha kodi ya centi 18.4 kwa galoni moja halitoshi.

“Naelewa sana kwamba kusitisha kwa muda tozo ya kodi ya mafuta pekee haitamaliza tatizo lakini itazipa familia afueni ya haraka, nafuu kidogo, wakati tunaendelea kufanya kazi ili kupunguza bei ya mafuta kwa muda mrefu,” Biden amesema.

Rais ameyataka pia majimbo kusitisha kwa muda tozo ya kodi ya mafuta, ambayo mara nyingi iko juu zaidi kuliko kodi ya serikali kuu.

Ameomba pia kampuni kubwa za mafuta kutoa mapendekezo juu ya jinsi ya kurejesha uwezo wa viwanda vya kusafisha mafuta watakapokutana leo Alhamisi na waziri wa nishati Jennifer Granholm.

The post Biden alitaka Bunge kusitisha kwa muda kodi ya mafuta ya petroli appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/27086/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT