Skip to main content

Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan ametangaza kufanya maandamano ya amani dhidi ya serikali

Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan, Imran Khan alitangaza Jumapili kwamba ataongoza maandamano ya amani dhidi ya serikali kwenye mji mkuu wa nchi hiyo Islamabad baadae wiki hii kushinikiza madai yake ya uchaguzi mpya.

Khan aliwaomba wafuasi wa chama chake cha Pakistan Tehreek-e-Insaf (PTI) na wa-Pakistan kwa ujumla kufika mjini ili kujiunga na mkutano wake unaoanza Jumatano akisema hatimaye utageuka kuwa maandamano ya kkupinga na kuendelea kushinikiza hadi matakwa yake yatakapotekelezwa.

Muungano unaoongozwa na upinzani ulimuondoa madarakani mchezaji huyo wa zamani wa Kriketi aliyegeuka kuwa mwanasiasa aliondolewa madarakani mwezi uliopita katika kura ya bunge ya kutokuwa na Imani nae na hivyo kuhitimisha serikali yake iliyodumu kwa takribani miaka mine. Mpinzani mkubwa wa Khan wa kisiasa, Shehbaz Sharif, alichukua nafasi yake kama mkuu wa muungano mpya unaotawala.

“hatutaikubali kamwe katika hali yoyote serikali hii, Khan aliuambia mkutano wa wanahabari kwa njia ya televisheni katika mji wa kaskazini-magharibi wa Peshawar wakati akitangaza mpango wake wa maandamano hayo. Aliionya mamlaka dhidi ya kuzuia kwa nguvu maandamano hayo. Kubaki Islamabad tutabaki huko hadi watakapovunja mabunge hayo na kutangaza tarehe ya uchaguzi wa wazi ambao hautaingiliwa na mataifa ya kigeni”.

Waziri wa habari Marriyum Aurangzeb alikosoa wito wa Khan wa maandamano na kukataa ombi lake la uchaguzi wa mapema akisema hawezi kudhulumu serikali kutangaza uchaguzi mkuu kwa wakati anaopenda kwa vitisho vyake.

Aurangzeb alisema uchaguzi mpya utatangazwa na serikali yake kwa ushirikiano na makubaliano na washirika wote.

The post Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistan ametangaza kufanya maandamano ya amani dhidi ya serikali appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/17556/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT