Skip to main content

Ukraine imefanya mashambulizi mapya Jumapili katika mji wa Kherson

Ukraine ilifanya mashambulizi mapya Jumapili ya kurudisha ardhi karibu na mji wa bandari wa kusini wa Kherson.

Vikosi vya Russia vililenga maeneo huko mashariki mwa Ukraine katika jaribio la kuuteka mji wa Sievierodonetsk mji wa mwisho unaodhibitiwa na Ukraine katika mkoa wa Luhansk.

Kherson unatumika kama uwanja wa kuyatayarisha majeshi ya Russia huko kusini mwa Ukraine mji wa kwanza mkubwa kuangukia kwa wanajeshi wa Moscow waliposonga kaskazini kutoka Crimea zaidi ya miezi mitatu iliyopita.

Lakini Jumapili jeshi la Ukraine lilisema kwenye Twitter subirini Kherson tunakuja. Wakati huo huo Sievierodonetsk ilikuwa lengo kuu la mashambulizi ya Moscow na sasa iko katika mashambulizi makubwa.

Gavana wa eneo la Luhansk ambalo ni pamoja na Donetsk linalounda mkoa wa Donbas alisema Ijumaa kwamba wanajeshi wa Russia wameingia Sievierodonetsk.

Kama Russia ingefaulu kuchukua maeneo haya kuna uwezekano mkubwa ikaonekana kuwa Kremlin imepata mafanikio makubwa ya kisiasa na kuonyeshwa kwa watu wa Russia kama kuhalalisha uvamizi huo wizara ya ulinzi ya Uingereza ilisema Jumamosi.

The post Ukraine imefanya mashambulizi mapya Jumapili katika mji wa Kherson appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/19728/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT