Skip to main content

Uchaguzi wa rais Somalia kufanyika Jumapili

Hali ya mvutano umeshuhudiwa nchini humo tangu kumalizika kwa muhula wa rais aliyeko madarakani mwaka jana bila kufanyika kwa zoezi hilo. mamlaka ya uchaguzi imeorodhesha wagombea 39 wakiwemo rais wa sasa Mohamed Abdullahi Mohamed, wengine wawili waliowahi kuwa marais, mmoja aliyewahi kuwa waziri mkuu, maafisa wa ngazi za juu pamoja na mwanahabari mmoja miongoni mwa wengine.

Vile vile kuna mwanamke mmoja kwa jina Fawzia Yusuf Haji Adam ,ambaye ni mbunge aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya kigeni nchini humo.Uchaguzi huo unafanyika wakati usalama ukiwa umedorora kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kundi la kigaidi la al Shabab linalopinga serikali , kwenye mji mkuu pamoja na maeneo mengine nchini. Shambulizi la kujitoa muhanga la Jumatano liliua takriban watu wanne wakiwemo wanajeshi wawili wa serikali kwenye kituo kimoja cha ukaguzi karibu na uwanja wa ndege wenye ulinzi mkali, ambapo wabunge watakutana Jumapili, ili kuchagua rais mpya.

The post Uchaguzi wa rais Somalia kufanyika Jumapili appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/SfKYiGa

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT