Skip to main content

Senegal imewazika watoto wachanga 11 waliokufa kwa ajali ya moto hospitalini

Senegal hapo Jumapili ilifanya mazishi ya watoto 11 ambao walikufa kutokana na moto uliowaka kwenye jengo la hospitali, Meya wa eneo hilo alisema baada ya mkasa huo kuibua hasira mpya juu ya hali ya mfumo wa afya.

Moto uliozuka Jumatano jioni katika mji wa magharibi wa Tivaouane ulikuwa wa hivi karibuni katika mfululizo wa vifo vya hospitali ambavyo vimefichua udhaifu wa mfumo wa afya wa Senegal.

Rais wa Senegal Macky Sall siku ya Alhamis alimfukuza kazi waziri wake wa afya lakini kwa wa-Senegali wengi hiyo haitoshi na wanaogopa majanga zaidi kutokea katika siku zijazo.

Mwezi uliopita mwanamke mjamzito alikufa kwa uchungu baada ya kuomba afanyiwe upasuaji lakini alikataliwa katika hospitali ya umma katika mji wa kaskazini-magharibi wa Louga.

Watoto 11 waliofariki katika ajali ya moto siku ya Jumatano kwenye wadi ya watoto wachanga walizikwa baada ya sala ya pamoja kwenye makaburi ya Tivaouane kulingana na matakwa ya familia zilizopoteza wapendwa wao. Mazishi hayo yalifanyika kwa faragha, Meya wa Tivaouane, Demba Diop Sy aliliambia shirika la habari la AFP.“Tunaomboleza uchungu walio nao wana familia, aliongeza. Leo ni siku ya mama nchini Senegal, na kuna kina mama 11 ambao wamepoteza watoto wao”.

Hitilafu ya umeme imetajwa kuwa chanzo cha moto huo katika hospitali ya Mame Abdou Aziz Sy Dabakh.

The post Senegal imewazika watoto wachanga 11 waliokufa kwa ajali ya moto hospitalini appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/qycxdj6

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT