Skip to main content

Russia yasema, juhudi za nchi za G7 kuitenga kiuchumi zimesababisha uhaba mkubwa wa chakula duniani

Mawaziri wa mambo ya nje wa G7 Jumamosi waliahidi kuimarisha kutengwa kwa Russia kiuchumi na kisiasa, kuendelea kuipa silaha Ukraine na kufanya kazi pamoja ili kupunguza uhaba wa chakula uliosababishwa na uvamizi wa Russia wa Februari 24 dhidi ya jirani yake.

“Majaribio ya kuitenga Russia kiuchumi, kifedha na upande wa usafirishaji kutoka kwenye njia za muda mrefu za ushirikiano wa kimataifa yanafanya mzozo wa kiuchumi na chakula kuwa mbaya zaidi,” wizara ya mambo ya nje ya Russia imesema katika tovuti yake.

“Izingatiwe kuwa ni hatua za upande mmoja za nchi za magharibi, hasa kutoka kundi la G7, ambalo limezidisha tatizo la kutotumia tena njia za kawaida za usafirishaji wa bidhaa na mifumo ya fedha kwa ajili ya usambazaji wa chakula kwenye masoko ya dunia,” wizara hiyo imeongeza.

Kabla ya vita, Ukraine na Russia pamoja zilikuwa zinazalisha asilimia 29 ya ngano kwa ajili ya soko la dunia.

The post Russia yasema, juhudi za nchi za G7 kuitenga kiuchumi zimesababisha uhaba mkubwa wa chakula duniani appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/DSIP6EN

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT