Skip to main content

REAL MADRID MABINGWA LIGI YA MABINGWA ULAYA


REAL Madrid wametwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuitungua bao 1-0 Liverpool kwenye mchezo wa hatua ya fainali iliyochezwa Uwanja wa de France.

Licha ya Liverpool kuwa na matumaini ya kuweza kulipa kisasi cha mwaka 2018 walipokutana kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Real Madrid kuweza kushinda bado wakati huu wameshindwa kwa mara nyingine tena.

Bao pekee la ushindi lilifungwa na Vinicius Junior ilikuwa dk ya 59 lilitosha kuwahakikishia ubingwa Real Madrid.

Rekodi zinaonyesha kuwa Real Marid waliweza kupiga mashuti mawili pekee ambayo yalilenga lango huku Liverpool ikipiga jumla ya mashuti 9 ambayo yalilenga lango.

Mchezo huo ulichelewa kuanza kutokana na sababu ya mashabiki wa Liverpool kuwa kwenye kashkashi wakati wa kuingia ndani ya uwanja kuweza kushuhudia mchezo huo jambo lililofanya uweze kuchelewa kuanza.

The post REAL MADRID MABINGWA LIGI YA MABINGWA ULAYA appeared first on Saleh Jembe.

The post REAL MADRID MABINGWA LIGI YA MABINGWA ULAYA appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/rYThGNX

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT