Skip to main content

RC Mwanza amtaka CAG Nyamagana

Na Clara Matimo, Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel, amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo, Ngusa Samike, amuandikie barua Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere kwenda mkoani humo kufanya ukaguzi wa kina kutokana na upotevu wa zaidi ya Sh Bilioni 3.15 zinazotolewa na serikali kwa makundi maalum katika Halmashauri ya Jiji hilo.

Mhandisi Gabriel ametoa maagizo hayo Mei 30, 2022 jijini humo kufutia taarifa aliyopewa na Kamati Maalum aliyoiunda mwezi mmoja uliopita kuchunguza ukiukwaji wa sheria, kanuni na taratibu katika kutoa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wajasiriamali kutoka makundi maalum ya vijana wanawake na watu wenye ulemavu.

Alisema  kamati hiyo ilitembelea Kata 10 kati ya 18 zilizomo ndani ya halmashauri hiyo na vikundi 156 kati ya 337 ndipo ilipobaini Sh bilioni 1.9  ziliidhinishwa na kamati ya huduma na mikopo  kwa miaka mitatu mfululizo  ingawa kwa mujibu wa  mweka hazina wa halmashauri ya jiji la Mwanza zilizotolewa ni Sh bilioni 5.2.

“Hivyo kwa maelezo hayo kamati imebaini kwa miaka mitatu mfululizo  kiasi cha Sh bilioni 3.15 zilitolewa bila kufuata utaratibu, hizo ni kata 10 tu ambazo kamati imetembelea imebaini ubadhilifu mkubwa kiasi hiki, je ingetembelea kata zote 18 zenye vikundi 680 sijui upigaji ungefika kiasi gani,” amehoji na kuongeza:

“Haya yote yanatokea lakini tunaye Mkaguzi wa ndani kama jicho lake halioni kama kanuni, taratibu na sheria zinavunjwa kwenye  utoaji wa mikopo ya  asilimia 10 inabidi CAG aje atusaidie kufanya ukaguzi maalum na wa kina, ripoti yake itatusaidia kuchukua hatua sahihi,” amesema Mhandisi Gabriel.

Amefafanua kwamba wakati wakimsubiri CAG kwenda kufanya ukaguzi huo, taratibu zingine kwenye matumizi ya fedha zitaendelea kwa mujibu wa sheria huku akiomba sekretarieti kuwepo na mfumo wa kidigitali nchi nzima au kila mkoa wa kuripoti na kurekodi taarifa zote za utaratibu na mchakato  wa vikundi kutoka makundi maaalum vinavyokopeshwa fedha za asilimia 10.

Aidha, Mhandisi Gabriel ameruhusu mikopo hiyo kuanza kutolewa katika halmashauri zote mkoani humo baada ya kusitisha Aprili 25, mwaka huu ili elimu ya kanuni, sheria na taratibu za mikopo hiyo itolewe kwa waratibu na wakopaji lengo likiwa ni kuimarisha usimamizi wa fedha na kutathmini utelelezaji wa kanuni hizo kutoka serikali za mitaa.

The post RC Mwanza amtaka CAG Nyamagana appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/19938/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT