Skip to main content

Rais Samia atajwa watu 100 wenye ushawishi mkubwa duniani 2022

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amechaguliwa na Jarida maarufu duniani la Times la nchini Marekani kuwa ni mmoja wa watu wa 100 wenye ushawishi mkubwa duniani kwa Mwaka 2022.

Rais Samia ambaye aliingia madarakani mwaka Machi, 2021 kufuatia kifo cha ghafla cha Rais John Pombe Magufuli amechaguliwa kwenye kundi la viongozi wenye ushawishi mkubwa kwa sasa duniani.

Wengine kwenye kundi hilo ni pamoja na Rais wa Marekani Joe Biden, Putin wa Urusi, Zelensky wa Ukraine, Xi Jinping wa China, Rais wa Umoja wa Ulaya, Ursula Von der Leyen, Kansela wa Ujerumani, Olaf Scholz, Letitia James ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa New York kutoka Chama cha Democratic pamoja na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Aby Ahmed.

Akimuelezea rais Samia baada ya uteuzi huo, Rais wa zamani wa Liberia Helen Sirleaf Johnson alisema toka achukue madaraka amefanya mabadiliko makubwa.

“Milango imefunguliwa kwa ajili ya majadiliano na maridhiano miongoni mwa mahasimu wa kisiasa, hatua zimepigwa katika kujenga upya imani ndani ya mfumo wa kidemokrasia, juhudi zimefanyika katika kuongeza uhuru wa habari na wanawake na wasichana hivi sasa wanaye mtu mpya mustakhbal wa maisha yao yaani mtu wa kuigwa(Role model)” alisema Rais hiyo zamani wa Liberia.

Amesema Septemba 21, mwaka jana Rais Samia alikuwa rais wa tano mwanamke kutoka Afrika kulihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na kutoa hotuba nzito.

“Alisimama katika mahali(podium) ambapo mimi nilisimama miaka 15 iliyopita nikiwa Rais wa kwanza mwanamke kutoka Afrika kulihutubia Baraza la Umoja wa Mataifa,” amesema na kuongeza:

“Rais Samia alisema hapa na mnukuu: ‘Nikiwa Rais wa kwanza mwanamke nchini mwangu, nabeba mzigo mzito wa matarajio ya kuleta usawa wa jinsia’ mwisho wa kumnukuu. Wakati anazungumza maneno haya mazito kabisa nilijikuta nikifikiri na kuwaza nguvu za mabega ya viongozi wanawake kubeba dhima hiyo na kwa umbali gani wataweza kutoa matokeo chanya,” amesema Sirleaf ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel.

The post Rais Samia atajwa watu 100 wenye ushawishi mkubwa duniani 2022 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/18169/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT