Skip to main content

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe amekemea tabia ya baadhi ya vijana wa chama hicho…

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe amekemea tabia ya baadhi ya vijana wa chama hicho ya kuwakosea heshima
watu ambao wanakuwa na mawazo tofauti na mawazo yao na kusema jambo hilo si la kiungwana.

Mbowe ameeleza hayo mkoani Dar es Salaam wakati akifungua kikao cha Baraza kuu la chama hicho.

Amesema ni vema vijana wa CHADEMA wanaofanya vitendo hivyo wabadilike na wawe na heshima na staha hata kwa watu wanaotofautiana nao kifikra hasa wanapokutana katika mitandao ya kijamii.

Mwenyekiti huyo wa CHADEMA Taifa amesema, kwa sasa chama hicho ndio chama kikuu cha upinzani nchini lakini haina maana kuwa siku zote ķitabaki katika nafasi hiyo.

Amesema unaweza ukafika muda kwa chama kingine cha siasa kuwa chama kikuu cha upinzani, hivyo hakuna maana yoyote ya kudhalilisha vyama vingine vya siasa na wanasiasa wengine.

Kikao hicho cha Baraza Kuu la CHADEMA kinahudhuriwa na Wajumbe takribani mia nne kutoka Tanzania Bara na Zanzibar.




Title of the document



The post Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe amekemea tabia ya baadhi ya vijana wa chama hicho… appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/13983/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT