Skip to main content

Mkuu wa jeshi la Sudan ameondoa hali ya dharura iliyowekwa tangu mapinduzi 2021

Mkuu wa jeshi la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan siku ya Jumapili aliondoa hali ya dharura iliyowekwa tangu mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 2021 baraza kuu linalotawala lilisema.

Burhan alitoa amri ya kuondoa hali ya dharura nchi nzima, baraza hilo lilisema katika taarifa yake. Agizo hilo lilitolewa ili kutayarisha mazingira ya mazungumzo yenye matunda na yenye maana ambayo yatafikia utulivu katika kipindi cha mpito, iliongeza taarifa.

Uamuzi wa Jumapili ulikuja baada ya mkutano na maafisa wa kijeshi kupendekeza hali ya hatari iondolewe na watu waliozuiliwa chini ya sheria ya dharura waachiliwe.

Pia imekuja baada ya wito wa karibuni uliotolewa na mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa, Volker Perthes wa kuondoa hali ya dharura kufuatia mauaji ya waandamanaji wawili wakati wa maandamano yanayopinga mapinduzi hapo siku ya Jumamosi.

Sudan imekumbwa na maandamano makubwa tangu mapinduzi ambayo yamekabiliwa na msako mkali ambao umesababisha takribani watu 100 kuuawa na mamia kujeruhiwa kulingana na wahudumu wa afya wanaounga mkono demokrasia.

The post Mkuu wa jeshi la Sudan ameondoa hali ya dharura iliyowekwa tangu mapinduzi 2021 appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/qycxdj6

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT