Skip to main content

Mkoa wa Geita kuendeleza ushirikiano na Waandishi wa Habari

Na Anna Ruhasha, Geita

Serikali mkoani Geita imeuhakikishia Umoja wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoani humo(GPC ) kuendeleza ushirikiano nao katika kuhabarisha umma masuala mbalimbali ya maendeleo ndani ya mkoa huo.

Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mkuu wa Mkoa huo, Rosemary Senyamule katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari ambapo klabu ya waandishi wa habari mkoani Geita imeazimisha Mei 16, mwaka huu Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Said Nkumba amesema Serikali inatambua mchango wa waandishi wa habari ambapo amesema wataendelea kushirikiana nao kwa karibu.

Aidha, Nkumba ametumia siku hiyo kuwataka waandishi wa habari mkoani humo kupendana na kufanyakazi kwa ushirikiano pasipo kujiona bora kuliko wengine katika ufanyaji kazi wa kuhabarisha umma.

Baadhi ya washiriki katika siku hiyo akiwemo Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita, SACP Henry Mwaibambe amewaomba waandishi wa habari kuandika habari za uchunguzi hasa za matukio ya mauaji.

“Nimpongeze Mwenyekiti wa klabu yenu, Renatus Masuguliko kunatukio lilitokea la mauaji huko vijijini alilifuatilia kwa kina na habari yake pia ililisaidia jeshi la polisi, niwaombe pia wengine mchunguze kwanza kabla ya kuandika, japo ni baadhi tu ya waandishi ambao wanaandika bila kijiridhisha kwa kina,” alisema SACP MMwaibambe.

Upande wake, Renatus Masuguliko akizungumza kwa niaba ya wanachama amesema kuwa Chama cha waandishi wa habari kinachotambulika kwa mujibu wa sheria ni kimoja kwa mkoa wa Geita ambacho ni GPC, hivyo ameiomba mialiko inayotolewa na Serikali kwa wandishi ipitie katika ofisi hiyo.

“Mgeni rasmi tukuombe kunamialiko mbalimbali inatolewa lakini haipiti ofisini kwetu, klabu hii inatambulika na imesajiliwa kisheria na waandishi wananchama ni waandishi wenye sifa tuombe hilo lifanyiwe kazi,” amesema Masuguliko.

The post Mkoa wa Geita kuendeleza ushirikiano na Waandishi wa Habari appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/8QeaTtN

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT