Skip to main content

Mbunge Makete achangia mjadala mfumuko bei ya mafuta

NA MWANDISHI WETU, Mtanzania Digital

MBUNGE wa Jimbo la Makete, Festo Sanga amesimama Bungeni kuchangia mjadala wa mfumuko wa bei ya mafuta na kusema suala hilo si dogo litaathiri maisha ya watu.

“Bei ya mafuta duniani hadi yanafika Dar es Salaam ni Tsh 1,162 kwa lita lakini msalaba na mnyororo wa kodi na tozo ni zaidi ya 1,300, yaani bei ya mafuta duniani ni ndogo kuliko mnyororo wa kodi tulizonazo, mimi niombe Serikali kuona umuhimu wa kupunguza hizi kodi.

“Suala la mafuta sio jambo dogo, ni jambo kubwa ambalo linaathiri kuanzia maisha ya mtu wa chini kabisa hadi wa mwisho, niwaombe Serikali hata kama tupo kwenye mazungumzo kwenye vikao tunavyoendelea navyo hili jambo ni la dharura lazima tulichukue katika udharura wake.

“Tozo ni nyingi sana, zipunguzwe kwa udharula tulio nao ili kunusuru msalaba wa ugumu wa maisha ya Watanzania hivi sasa. Serikali itafute fedha mahali pengine kwa ajili ya kuweka ruzuku kwenye mafuta ili bei ishuke.

“Hali ya maisha imekuwa ngumu, mafuta yanamnyororo mrefu kwenye bidhaa na huduma mbalimbali. Yanapopanda yaaathiri kila sekta ya kiuchumi,” amechangia Sanga.

The post Mbunge Makete achangia mjadala mfumuko bei ya mafuta appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/12289/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT