Skip to main content

Marekani inawakaribisha viongozi wa Amerika Kusini kwenye mkutano wa bara la Amerika

Marekani ilisema Jumatatu inatafuta njia za kuwawakilisha watu wa Cuba, Venezuela na Nicaragua katika mkutano wa kilele mwezi ujao kufuatia vitisho vya kususia kutengwa kwa serikali zao.

Marekani inawakaribisha viongozi wa Amerika Kusini mjini Los Angeles kwa ajili ya mkutano wa bara la Amerika kuanzia June 6 hadi 10 ikiwa ni sehemu ya juhudi za Rais Joe Biden kuhamasisha demokrasia na kukabiliana na uhamiaji, pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa.

Maafisa wa marekani walisema kwamba waliyataarifu rasmi mataifa hayo wiki iliyopita , na kwamba mialiko zaidi itafuata.

“Bado tunatathmini chaguo la namna ya kujumuisha vyema sauti za watu wa Cuba, Venezuela na Nicaragua katika mchakato wa mkutano huo” afisa katika utawala alisema.

Wizara ya mambo ya nje hapo awali, ilielezea Imani katika ushiriki imara huko Los Angeles bila ya kufichua orodha ya mwaliko.

Afisa wa cheo cha juu kwa Latin America, Brian Nicols awali alisema hatarajia mialiko kwa maafisa kutoka Cuba, Nicaragua, na Venezuela kwa vile serikali zao haziheshimu mkataba wa mwaka 2001 wa Inter-American Democratic Charter.

Lakini Cuba ilialikwa kwenye mikutano ya kilele hapo mwaka 2015 huko panama na mwaka 2018 huko Peru. Tangu wakati huo Biden amekuwa akifanya mabadiliko ya mtangulizi wake Donald Trump kwa Marekani kufungua tena shughuli zake kwenye kisiwa hicho kinachoendeshwa kikomunisti.

Rais wa Mexico, Andres Manuel Lopez Obrador ambaye ni mrengo wa kushoto anatishia kususia mkutano huo kama Marekani haitazialika nchi zote.

Tangu wakati huo viongozi wa Argentina, Bolivia, Honduras na Jumuiya ya Mataifa 14 ya Caribbean pia wameweka ushiriki wao mashakani huku Chile ikijiunga na wito kwa uwezekano mkubwa wa kushiriki.

The post Marekani inawakaribisha viongozi wa Amerika Kusini kwenye mkutano wa bara la Amerika appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/NbcCBIR

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT