Skip to main content

Kundi la Islamic State limedai kuhusika na shambulizi la DRC lililouwa watu 15

Islamic State siku ya Jumanne lilidai kuhusika na shambulizi lililoua takribani raia 15 katika kijiji kimoja kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo siku ya Jumapili. Kundi hilo la wanamgambo lilisema kwenye mtandao wake wa mawasiliano ya telegram.

Kundi la kutetea haki za binadamu na afisa mmoja wa eneo hilo alisema Jumatatu kwamba wapiganaji wanaoaminika kuwa wanachama wa Allied Democratic Forces (ADF) walivamia kijiji cha Bulongo katika jimbo la Kivu kaskazini, baada ya kiza kuingia siku ya Jumapili na kuharibu nyumba pamoja na kuwaua wakaazi ambapo walipita kwenye njia yao na kuchoma moto magari sita.

ADF ni wanamgambo wa Uganda ambao wamekuwa wakiendesha harakati zao mashariki mwa Congo tangu miaka ya 1990 na kuua raia wengi ambapo wengi wao ni katika mashambulizi ya usiku wa manane yaliyofanywa kwa kutumia mapanga na mashoka.

Pia kundi liliahidi ushirika na Islamic State mwaka 2019. Islamic State ilidai kuwa wanachama wake waliwauwa takribani wakristo 20 na kuchoma moto malori sita katika shambulizi hilo kwa kutumia bunduki za rashasha na kurejea katika vituo vyao bila kuumia.

The post Kundi la Islamic State limedai kuhusika na shambulizi la DRC lililouwa watu 15 appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/4tiPUgR

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT