Skip to main content

Kiongozi wa Taliban nchini Afghanistan anaahidi nchi hiyo haitakuwa tena tishio kwa Marekani

Kiongozi wa cheo cha juu wa utawala wa Taliban nchini Afghanistan anaahidi nchi yake kamwe haitakuwa tena tishio la kigaidi kwa Marekani na aliahidi habari njema hivi karibuni juu ya kurejea kwa wanawake na wasichana wa Afghanistan katika shule za sekondari. Kaimu Waziri wa Mambo ya Ndani Sirajuddin Haqqani pia Naibu Mkuu wa Taliban alisisitiza tena uhakikisho huo katika mahojiano nadra na Christiane Amanpour wa CNN yaliyotangazwa Jumatatu.

Kundi la Taliban lilipata tena mamlaka baada ya wanajeshi wa Marekani na NATO kujiondoa katika taifa hilo la Asia Kusini lililokumbwa na vita hapo Agosti mwaka 2021 na lilianzisha serikali ya mpito ya wanaume pekee ikiita Imarati ya Kiislam ya Afghanista (Islamic Emirate of Afghanistan).

Kundi hilo lenye msimamo mkali liliwaruhusu wanafunzi wa kike wa chuo kikuu kurejea chuoni katika mfumo mpya ulioelezewa wa elimu unaotenganisha jinsia. Lakini licha ya kuahidi mara kwa mara kuwaruhusu wasichana wa Afghanistan kurudi kwenye madarasa yao Taliban bado hawajafungua tena shule za sekondari kwa wasichana.

The post Kiongozi wa Taliban nchini Afghanistan anaahidi nchi hiyo haitakuwa tena tishio kwa Marekani appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/XYWwbU4

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT