Skip to main content

Jeshi la DRC lathibitisha kuwashilikia wanajeshi wawili wa Rwanda

Jumamosi, Rwanda ilidai kuwa wanajeshi wake wawili walitekwa nyara na waasi wa Kihutu wanaoendesha harakati zao mashariki mwa DRC.

Lakini jeshi la DRC lilisema wanajeshi hao walivuka mpaka na kuingia kwenye ardhi ya Congo na wamezuiliwa na wenyeji.

Kila serikali huishutumu nyingine mara kwa mara kuunga mkono makundi ya waasi ambayo inataka kuyatokomeza.

Brigadia Jenerali Sylvain Ekenge amesema kukamatwa kwa wanajeshi hao wawili ni ushahidi kuwa jeshi la Rwanda linaendesha operesheni zake kwenye ardhi ya Congo.

“Kulingana na maelezo ya wanajeshi hao, waliingia kwenye ardhi ya Congo Jumatano tarehe 25 Mei kushambulia kambi ya jeshi la Congo ya Rumangabo, umbali wa zaidi ya kilomita 20 kutoka mpaka wa Rwanda,” Ekenge amesema.

“Baada ya kufurushwa na jeshi la DRC huko Rumangabo, walipotea na hatimaye walikamatwa na wenyeji, amesema Ekenge ambaye ni msemaji wa jeshi katika jimbo la Kivu Kaskazini, ambako Rumangabo inapatikana.

Jeshi la Rwanda lilitoa wito kwa viongozi mjini Kinshasa kufanya wawezalo ili wanajeshi wake waachiliwe, likisema walitekwa nyara wakati wakifanya doria ya kuwasaka waasi wa Rwanda wa kundi la Kihutu la Democratic Forces for the Liberation of Rwanda( FDLR) na baadaye wakachukuliwa na kuvushwa mpaka ndani ya DRC.

The post Jeshi la DRC lathibitisha kuwashilikia wanajeshi wawili wa Rwanda appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/19722/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT