Skip to main content

IBEC: Musyoka hatashiriki kinyang’anyiro cha uchaguzi wa rais Agosti 9

Wakati huo huo, Tume Huru ya Uchaguzi (IEBC) imewapitisha wagombea 16 ambao hivi sasa watawasilisha nyaraka zao za uteuzi wao kuanzia Jumamosi.

Orodha hiyo ina wagombea watarajiwa 9 wa vyama vya siasa au muungano wa vyama vya kisiasa na wagombea saba huru.

Wagombea wanaoongoza Raila Odinga wa Azimio la Umoja (One Kenya Coalition party) na Naibu Rais William Ruto wa Chama cha United Democratic Alliance ni kati ya waliopitishwa na IEBC.

Bwana Musyoka hakuwasilisha orodha ya wafuasi wake katika waraka wa Microsoft Excel.

Yeye ni miongoni mwa wagombea wanne wa vyama vya siasa na tisa wagombea huru walioshindwa kukidhi matakwa ya IEBC ya kupata wafuasi 48,000 na angalau kaunti 24, kuwasilisha majina ya wafuasi hao pamoja na nakala ya vitambulisho vyao vya kitaifa.

Kwa Bw Musyoka, kushindwa kwake kuvuka kiunzi cha kwanza kunahitimisha safari yake ya ugombea urais ambayo ilianza baada ya kushindwa kupata nafasi ya mgombea mwenza wa Chama cha Azimio.

Hata kabla ya kujulikana kuwa amezuiwa kushiriki katika kinyang’anyiro hicho na IEBC, wafuasi wa Bw Musyoka na wagombea wa Wiper walikuwa wanaweka shinikizo kwake kurejea katika chama cha Azimio na kuwaunga mkono Odinga -Martha Karua.

Hivi sasa yeye hana hiari kwani kisheria hawezi tena kutoka Azimio.

Lakini tayari yuko mashakani wakati akijaribu kujiunga tena na chama cha Azimio la Umoja One Kenya Coalition.

The post IBEC: Musyoka hatashiriki kinyang’anyiro cha uchaguzi wa rais Agosti 9 appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/19478/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT