Skip to main content

DRC yaishtumu Rwanda kuunga mkono waasi wa M23

Mapigano na kundi hilo la waasi yalizuka kwenye maeneo mengi wiki hii katika mkoa wa Kivu Kaskazini unaopakana na Rwanda.

“Tuhuma zinaonyesha kuwa M23 ilipata uungwaji mkono wa Rwanda,” msemaji wa serikali ya Congo Patrick Muyaya alisema Jumatano jioni, baada ya mkutano wa dharura na waziri mkuu.

M23 ni moja ya zaidi ya makundi 120 yenye silaha ambayo yanapatikana mashariki mwa DRC.

Kundi hilo liliwahi kuuteka kwa muda mfupi mji wa mkoa wa Kivu Kaskazini, Goma mwishoni mwa mwaka wa 2012, kabla ya jeshi kutokomeza uasi mwaka uliofuata.

Lakini M23 ilianzisha tena mapigano mwaka huu, ikiishtumu serikali ya Congo kushindwa kuheshimu makubaliano ya mwaka wa 2009 ambayo yalieleza kuwa wapiganaji wake wangepaswa kujumuishwa katika jeshi la taifa.

Waziri wa mambo ya nje wa DRC Christophe Lutundula ameiishtumu pia Rwanda kuwasaidia waasi wa M23 akisema kwamba, kundi hilo la waasi lilishambulia kambi ya kijeshi ya Rumangabo, umbali wa kilomita 40 kaskazini mwa Goma.

Lakini Rwanda imekanusha kuhusika katika mzozo huo kati ya M23 na serikali ya Congo. Msemaji wa serikali ya Rwanda Yolande Makolo amesema nchi yake “haina nia ya kuingizwa katika suala la ndani la DRC”.

Mapigano kati ya jeshi la Congo na M23 yaliendelea Alhamisi karibu na kambi ya Rumangabo, vyanzo vya eneo hilo vimesema.

The post DRC yaishtumu Rwanda kuunga mkono waasi wa M23 appeared first on soka letu.

Via soka letu https://ift.tt/sBf6cEb

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT