Skip to main content

Bakwata, Meya wawakumbuka yatima, watoa wito kwa familia

Na Clara Matimo, Mwanza      

Jamii imetakiwa kuwakumbuka watoto na kuhakikisha wanalelewa na kukua katika malezi bora pale wanapopoteza wazazi wao kuliko kuwaza mali na kuwasababishia  kuishi kwenye mazingira hatarishi.

Wito huo umetolewa jijini Mwanza Mei 3, mwaka huu na Mstahiki Meya wa Jiji hilo, Costantine Sima, aliposhiriki  chakula cha pamoja na watoto  yatima, kilichoandaliwa  na Baraza  Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) Mkoa wa Mwanza kwa kushirikiana na mfanyabiashara Zacharia Nzuki.

Alisema serikali inasisitiza umuhimu wa familia kutowatelekeza watoto lakini ndugu, jamaa  kuwatunza watoto yatima kwa kuwa  inatambua  jamii yote inaowajibu wa kuendelea kuwatunza kwa sababu nafasi mbalimbali za uongozi wa baadaye zitashikiliwa na watoto wa sasa.

 “Katika ujenzi  wa taifa lolote duniani ni lazima tuwahusishe watoto wetu yatima wakiwemo, leo upo una nguvu kesho nguvu zitakuishia utawahitaji, kama utawaharibu leo ukubali matokeo  mabaya ya kesho hivyo  tushiriki kujenga misingi yao tangu wakiwa wadogo.

“Watoto msikubali kudanyanywa na watu wazima wenye lengo la kuwaharibia maisha,  ambao mmepata nafasi ya kwenda shule kazanieni masomo yenu sasa hivi kila kitu kinahitaji elimu, kukosa wazazi, kuishi katika mazingira magumu na kuugua hayo siyo mwisho wa maisha yenu,”alisema Sima.

Akizungumza kwa niaba ya watoto hao, mtoto Al Bidh  Yusuph, (13) aliisihi  jamii kuwapenda  yatima na kuwahudumia mahitaji muhimu wasibahirie walivyo navyo kwani wanavyovitoa watavikuta kwa Mwenyezi Mungu kama ambavyo Mtume Mohamed alivyosema  kwamba mtu yeyote atakayeshika kichwa cha  mtoto yatima  na kujua anahitaji huruma, Mwenyezi Mungu anamuandikia baraka na kumfutia dhambi zote alizozifanya kwa kila nywele moja ya mtoto yatima aliyoigusa.

Sheikh wa Mkoa wa Mwanza, Hasani Kabeke, aliwataka  waumini  wa dini ya kiislamu kuwajali, kuwalea, kuwalinda na kuwathamini  watoto yatima kwani hayo ni maagizo ya  Mtume Mohamed ndiyo maana Bakwata mkoani humo  imejiwekea utaratibu wa kulisha yatima  Idd Mosi ya kila mwaka kwa kuwa   Idd El Fitri ni sikukuu ya kula.

“Mtume wetu Mohamed  alisema yeyote atakayelea  watoto yatima vizuri atakuwa  naye ahera siku ya kiama na watoto yatima inatakiwa walelewe ndani ya familia zetu wakifiwa na wazazi wao bado wanao ndugu wengine upande wa mama zao na baba zao.

“Zamani mtu akifa ndugu wanachukua watoto wake,  leo baada ya kufikiri watoto wa marehemu watalelewa vipi, wanawaza kuwadhulumu mali za wazazi wao,  watanzania turudi kwenye utaratibu wa kulea watoto yatima tukifanya hivyo hatutakuwa na watoto wanaoishi mazingira hatarishi, “alisema Sheikh Kabeke.

Kwa upande wake Zacharia Nzuki, alisema amewaandalia chakula kwa ajili ya sikukuu ya Idd El Fitr watoto hao kwa sababu ni kundi linalogusa kaya za watanzania wote kwa namna moja au nyingine huku akiihamasisha jamii kutowanyanyasa wala kuwabagua na kila mwenye nafasi ashiriki katika malezi yao.

The post Bakwata, Meya wawakumbuka yatima, watoa wito kwa familia appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/12603/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT