Wakati Mataifa mbalimbali duniani yakiingia kwenye changamoto ya upatikanaji wa nishati ya mafuta na mfumuko wa Bei wa nishati h…
Wakati Mataifa mbalimbali duniani yakiingia kwenye changamoto ya upatikanaji wa nishati ya mafuta na mfumuko wa Bei wa nishati hiyo inayotokana na Vita kati ya Urusi na Ukraine, Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Ewura imeeleza kuwa bado Tanzania haijafikia kwenye hali Mbaya ya upatikanaji wa Mafuta.
Akizungumza katika Kikao kazi cha Mamlaka hiyo na Wahariri wa Vyombo vya Habari Jijini Dar es salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Ewura Mhandisi Godfrey Chibulunje amesema kwasasa Tanzania ina Hifadhi ya mafuta ya petrol yanayoweza kutumika kwa siku 28 nchini bila kuingiza mengine, wakati Hifadhi ya Diesel imebaki ya siku 19 huku Hifadhi ya mafuta ya Taa inaweza kutumika kwa siku 108 na mafuta ya Ndege ya siku 35 ikiwa ni zaidi ya wastani wa kidunia wa siku 15.
“Tusijione kama tupo kwenye hali Mbaya, bali ni mwenendo wa Dunia nzima, tumetoka kwenye changamoto za UVIKO 19, na Sasa Vita ya Urusi na Ukraine imesababisha adha kubwa kwenye sekta ya nishati ya mafuta ikizingatiwa kuwa Urusi ni mzalishaji mkubwa wa nishati hiyo duniani” Mhandisi Godfrey Chibulunje – Kaimu Mkurugenzi Ewura.
#StarTvUpdate

The post Wakati Mataifa mbalimbali duniani yakiingia kwenye changamoto ya upatikanaji wa nishati ya mafuta na mfumuko wa Bei wa nishati h… appeared first on soka letu.
source https://mjombazecoder.website/3308/
Comments
Post a Comment