Skip to main content

Tume ya mpito ya AU nchini Somalia yatarajia kupata kiongozi mpya

Tume ya mpito ya amani ya Umoja wa Afrika nchini Somalia inatarajia kupata kiongozi mpya katika siku zijazo baada ya uhusiano kati ya serikali iliyowapokea na mkuu wa tume ya ulinzi kuharibika wiki iliyopita.

Vyanzo vya kidiplomasia vimeliambia gazeti la The East African itakuwa ni “muhali” kwa Francisco Madeira kurejea Somalia baada ya nchi hiyo kumuondolea hadhi ya kidiplomasia.

Chanzo kilisema Bwana Madeira, raia wa Msumbiji, alikuwa anashinikizwa kujiuzulu ili isionekane kwamba alikuwa amefukuzwa kazi.

Bw Madeira alikuwa hajajibu maswali yetu.

Mkuu wa Tume ya mpito ya amani ya Umoja wa Afrika (Atmis) angelikuwa anasherehekea wiki chache za awali za chombo hicho kipya cha kulinda amani, baada ya Amisom, sehemu kubwa ni tume ya kijeshi iliyokuwa ikiwalenga al-Shabaab iliyodumu kwa miaka 13, imebadilishwa kwa kuletwa nyingine.

Kipindi cha mpito, hata hivyo, kimeenda sambamba na taarifa zilizotolewa kuwa Madeira aliingia katika matatizo na serikali ya Somalia baada ya sauti yake ilipobainika ikiwakashifu maafisa wa serikali kwa udhaifu wao wa kushughulikia matatizo ya usalama.

Kuanzia Alhamisi wiki hii Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat alikuwa akionyesha kusita waziwazi kuwa “ana imani kamili” na Bw Madeira, msimamo ulioungwa mkono na Rais wa Somalia Mohamed Farmaajo , lakini wakati Waziri mkuu wake Hassan Roble hakubaliani naye..

Siku ya Jumatatu, Bw Roble alitekeleza amri ya kufukuzwa Bw Madeira, ikiwemo kumoundolea hadhi ya kidiplomasia kama kutumia ukumbi wa VIP kwenye uwanja wa ndege, kufuta kibali chake cha kazi cha kidiplomasia na hadhi nyingine alizokuwa nazo wakati akihudumu kama mwakilishi maalum wa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika na mkuu wa Atmis.

Chanzo cha habari hii ni gazeti la The East African

The post Tume ya mpito ya AU nchini Somalia yatarajia kupata kiongozi mpya appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/6725/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT