Skip to main content

TanTrade wakutana na wadau wa ngozi nchini

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) imeratibu na kushiriki kikao cha wadau wa ngozi hapa nchini kilichowajumuisha wataalam kutoka Taasisi ya Ushirikiano ya Kijerumani (GiZ leather technical team).

Kikao hicho kilifanyika Aprili 26, 2022 kwa lengo la kujadili hatua za awali za utekelezaji wa Mradi wa ‘Support towards Industrialization and Productive Sectors’ ambapo sekta ya ngozi ni miongoni mwa zilizopewa kipaumbele.

Mradi huo utatekelezwa katika nchi wanachama wa SADC kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).

TanTrade iliwakilishwa na wataalam kadhaa wa sekta ya ngozi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara, Emmanuel Miselya, ambaye aliwaeleza wadau wa ngozi kuwa mamlaka hiyo ipo tayari kushirikiana nao kuhakikisha sekta hiyo inakua na kuleta tija kuanzia mfugaji hadi muuzaji wa bidhaa za ngozi.

Kwa upande wake mtaalam kutoka GiZ, Klaus Heinze, amesema sekta ya ngozi bado ina fursa kubwa kwa soko la ndani ya nchi na katika soko la SADC kwani bidhaa nyingi za ngozi zinaingizwa katika soko hilo kutoka mataifa ya mbali.

“Namna bora ya kuhakikisha sekta hii inakua ni kuhakikisha mnyororo wa thamani unasimamiwa ipasavyo kwa kila hatua,” amesema Heinze.

Naye Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Wazalishaji wa Bidhaa za Ngozi nchini, Freddy Kabala, alitaja baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo kuwa ni pamoja na ukosefu wa ngozi zenye ubora, utaalam duni wa uzalishaji pamoja na mitaji.

Amesema changamoto hizo zinasababisha bidhaa zinazozalishwa nchini kuonekana kuwa ghali na hivyo kupunguza uzalishaji na kutoa mwanya kwa bidhaa nyingi kutoka nje ili kuziba pengo kubwa lililopo.

Tanzania inakadiriwa kuwa na ng’ombe zaidi ya nilioni 33.4 na mifugo mingine kama mbuzi na kondoo zaidi ya milioni 30 wakati uzalishaji wa viatu vya ngozi ni wastani wa jozi milioni tatu huku jozi milioni 54.3 za viatu vya ngozi vikiingizwa nchini kutoka mataifa mengine ya Ulaya na Asia kwa mwaka.

Mpaka Sasa kuna viwanda vinne vikubwa vinavyozalisha bidhaa za ngozi nchini ambavyo ni Bora Industries, Woiso Original Products (WOP), Ital Shoes na Kilimanjaro Leather International Company Industries Ltd.

The post TanTrade wakutana na wadau wa ngozi nchini appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/9856/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT