Skip to main content

Petro de Luanda ya Angola yaishinda FAP ya Cameroon

Baada ya kushindwa Ijumaa usiku na Zamalek ya Misri, Petro de Luanda ya Angola ilirejea uwanjani Jumamosi na kushinda dhidi ya Forces Armées et Police Basketball- FAP ya Cameroon kwa jumla ya pointi 73-60.

Keumoe wa Cameroon alimpasia Byers ambaye aliurudisha kwa Keumoe naye alipachika pointi mbili za kwanza za mchezo huo.

Mabingwa hao wa Angola walijibu wakati Morais alipompasia Gakou ambaye aliweka mpira nyavuni.

Pedro wa Luanda alizidi kupanua uongozi wa timu yake alipofunga pointi mbili na kufanyiwa madhambi.

Domingos wa Petro alimpasia Paulo ambaye alikaribia kikapu lakini mpira wake ulizuiwa na Bidias wa FAP huku Toko akipata mpira wa uliorudi na kumpasia Bidias upande wa pili wa uwanja aliyepachika pointi mbili.

Zikiwa zimesalia dakika 2 kipindi cha kwanza kumalizika, Gonçalves wa Petro alimpasia Moreira aliyeingiza nyavuni kwa mkono mmoja.

Naye Bidias wa Cameroon alijaribu kupunguza uongozi wa Angola wa pointi 9 huku akipachika pointi mbili kwa timu yake.

Gakou wa Petro alimpasia Dundão ambaye alipachika pointi tatu, akiendeleza uongozi wao hadi pointi 10 katika kota ya 3.

Zikiwa chini ya dakika 10 kabla ya mchezo kumalizika, Joaquim wa Petro alimpasia Gonçalves ambaye alipiga pasi ya haraka kwa Pedro lakini alirudishiwa na kufunga pointi mbili.

Petro wakiwa juu kwa pointi 16 Gonçalves alimpasia Dundão aliyepachika pointi ya masafa marefu na kusukuma uongozi wao hadi pointi 19.

Na walimaliza mchezo huku Petro wakichukua ushindi kwa pointi 13 na kuandikisha ushindi wao wa tatu wa kanda ya Nile huku FAP wakipoteza mchezo kwa mara ya pili.

The post Petro de Luanda ya Angola yaishinda FAP ya Cameroon appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/6728/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT