Skip to main content

Peaktime Media yaahidi burudani kabambe ya masumbwi

NA WINFRIDA MTOI, Mtanzania Digital

UONGOZI wa kampuni ya Peaktime Media ambao ni waandaaji wa mapambano ya ngumi nchini, umehidi kutoa burudani kabambe kwa mashabiki wa masumbwi mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Meja Seleman Semunyu jana baada ya kufuturisha mabondia na wadau wa ngumi kwenye Ukumbi wa JWTZ (Club 361) uliopo Mwenge, Dar es Salaam.

Meja Semunyu amesema katika kuhakikisha burudani hiyo inawafikia Watanzania wengi, kwa mara ya kwanza historia itaandikwa Songea, mkoani Ruvuma ambapo pambano la kisasi ya marudiano litapigwa kati ya Selemani Kidunda na Erick Katompa Julai 30,2022.

Baadhi ya wadau waliojitokeza katika futari iliyoandaliwa na Peaktime Media jana

“Tulianza na Mfalme kwenye Ufalme wake(Twaha Kiduku Vs Alex Kabangu) Morogoro, sasa tutakwenda Songea kwenye Usiku wa Kisasi 2022 kati ya Kidunda na Katompa, pambano hili tayari Mkuu wa Majeshi ameshatoa kibali, naamini mtaendelea kuniunga mkono,” amesema.

Selemani Kidunda(kulia) na Erick Katompa(kushoto),waliopo vifua wazi walipokutana mwaka jana.

Meja Semunyu amefafanua kuwa tangu mwaka jana hadi sasa, wamefanikiwa kuandaa mapambano 10, hivyo anaamini wadau wa ngumi watazidi kumpa sapoti ili kufanikisha malengo waliyojiwekea katika kuendeleza mchezo wa masubwi.

Kwa upande wake, Kidunda amesema yeye yupo vizuri na anaendelea na mazoezi, huku makocha wake wakiendelea kumnoa na kurekebisha pale walipokosea, hivyo atahakikisha ubingwa unabaki nyumbani.

Baadhi ya wadau waliojitokeza katika futari iliyoandaliwa na Peaktime Media jana

“Tulilotaka liwe limekuwa, ndio kama hivi mnaona Mcongo anarudi tena, kama vile usemi wangu kuwa ‘Ajavyo ndivyo Tumpokeavyo’, naomba tushirikiane katika hii game tuwe pamoja kule Songea,” amesema

Kidunda na Katompa wanarudiana baada mwaka jana kushindwa kupatikana mshindi kutokana na pambano kusitishwa utokana na Kidunda kuumizwa kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza.

The post Peaktime Media yaahidi burudani kabambe ya masumbwi appeared first on soka letu.



source https://mjombazecoder.website/10566/

Comments

Popular posts from this blog

Dr. William Samoei Ruto: muuza kuku ambaye sasa ni rais wa Kenya

Ruto ameweka historia kwa kuwa mgombea wa kwanza wa urais katika Jamhuri ya Kenya kushinda kura za urais katika jaribio la kwanza. Amekuwa naibu wa kwanza wa rais kushinda kiti cha urais katika Jamhuri ya Kenya. Mwanasiasa ambaye hajawahi kushindwa katika uchaguzi wowote. Mwanasiasa ambaye ametajwa na wachambuzi kama mchapa kazi na mwenye bidii na kiu ya kupata kile anacholenga maishani. Mtu asiyekata tamaa. Mcheshi katika hotuba zake, anayesemekana kutaka kujua kila linaloendelea karibu naye, mtu mkarimu mwenye roho ya kuchangisha pesa kwa watu na kwa ajili ya miradi mbalimbali. Ruto ameshutumiwa kwa kashfa kadhaa hasa za ufisadi bila kesi kufikishwa mahakamani, na ameshinda karibu kesi zote ambazo zimewahi kufunguliwa mahakamani dhidi yake ikiwemo kesi katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC. Yafuatayo ndiyo mambo muhimu yanayomhusu rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya Dr. William Samoei Ruto. Majina Kamili: William Samoei Arap Ruto Umri: miaka 55 Mke wake: Rachel Chebet Ruto ...

Jioni

Download Audio The post Jioni appeared first on soka letu . source https://mjombazecoder.website/54168/

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye

Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kufuatia upigaji kura uliofanyika Jumapili mjini Mogadishu. Upigaji kura huo ulifanyika katika uwanja wa ndege wa Mogadishu uliokuwa na ulinzi mkali huku wanajeshi wa Umoja wa Afrika wakilinda hema la Afisyone ambalo lilikuwa ni sehemu ya kupigia kura. Katika kikao cha pamoja cha mabaraza mawili ya bunge yenye wajumbe 328 waliwapigia kura wagombea 36 wa urais katika duru tatu. Mohamud alimshinda Rais aliyekuwa madarakani Mohammed Abdullahi Mohamnmed maarufu kama “Farmaajo” katika duru tatu za upigaji kura. Hassan Sheikh Mohamud alikuwa rais kati ya Agosti 2012 na Februari 2017. The post Bunge la Somalia limemchagua tena Rais wa zamani Hassan Sheikh Mohamud kuwa rais ajaye appeared first on soka letu . Via soka letu https://ift.tt/ZmsWCwT